TAMU CHUNGU: Utekaji wa Cua mwaka 1998

 

Habari msomaji wangu, leo ninakuletea Makala hupi inayohusu utekaji wa mwaka 1998. Utekaji huu ulitokea tarehe 5 mwezi April mwaka 1998, katika mji wa Cúa, nchini Venezuela, ambapo kijana wa miaka 18 Hector Duarte Bahamonte alipokwenda kupora katika duka la mikate akiwa na bunduki aina ya revolver. Mpango wake huo wa utekaji haukufanikiwa, aliamua kuja na mpango mwingine akamchukua mwanamke mmoja kama mateka wake na kumtishia kumuua. Maamuzi hayo aliyachukua baada ya polisi kuwasili katika eneo la tukio ambapo aliwarushia risasi na ushikiriaji huo mateka ulidumu kwa masaa 7. Baadae polisi waliamua kufanya maamuzi magumu na hapo ndipo skari mmoja kutoka kikosi maalumu cha polisi akiwa na maski akafyatua risasi ambayo ilimpata Duarte kwenye kichwa. Duarte alidondoka chini na kupoteza maisha kisha mwanamke mateka akawa salama. Kifo chake kilinaswa na kamera.

Kama nilivyoeleza hapo awali kuwa tukio hili lilitokea katika mji wa Cúa, karibu kilometa 50 kutoka mji wa Caracas kusini, mji mkuu wa Venezuela. Duarte alipokwenda kufanya upora polisi walipata taarifa na walifika mara moja kwenye eneo la tukio na kumpiga risasi ya mkono. Mara baada ya kupigwa risasi ya mkono, Duarte alikimbilia katika nyumba moja ya makazi na kumteka mwanamke wa miaka 44 aliyeitwa Nancy López pamoja na familia yake. Duarte aliwafyatulia risasi mateka wawili, mmoja alikuwa mtoto wa kiume wa miaka 9, na kuwaacha wote wakivuja damu, hapo ilikuwa ni ghorofa ya 9. Kisha akatoka ndani akiwa na López. Alimuwekea revolver yake kichwani akitishia kumuua kama hata pata gari la kutorokea. Lengo la Duarte lilikuwa kupata gari na kukimbilia Caracas. Polisi walianza majadiliano na Duarte wakimshawishi kumuachia Lopez kisha wapatie gari lakini Duarte hakuwa mwepesi sana. Mkuu wa polisi Ivan Simonovis ndiye aliyekuwa anaendesha operesheni ya kumuokoa López.

Masaa saba yakakatika, polisi wakiendelea kufanya majadiliano na Duarte wakimsihi ajisalimishe kwa amani ili kupunguza madhara lakini bado Duarte hakukubali. Wakati wamajadiiano kati yake na Poilisi, Duarte aliweza kuongea na mama yake kwa kupitia simu ya polisi. Pamoja na kutishiwa kuuawa taarifa zinasema, López alikuwa mtulivu sana. Polisi walifanya kila jitihada kumshawishi Duarte kutatua tatizo lililokuwa linamka bili kwa njia ya amani lakini alikataa. Sehemu ya ripoti inasema, Duarte alisikika akisema "Mkiniua na mimi na muua huyu mwanamke. Nipelekeni makaburini mara moja. Leteni majeneza mawili". Baadae alifika mwanasaikolojia wa jeshi la polisi ambaye aliendelea na majadiliano na Duarte akiwa karibu na gari moja aina ya van, nyuma ya van hiyo alikuwepo mlenga shabaha mmoja. Ghafla polisi mmoja aliyekuwa na maski alifyatua risasi moja akitumia bunduki ya kulengea shabaha yaani sniper rifle, risasi ilimpata vyema Duarte katika jicho lake la kushoto. Duarte akadondoka chini na kufariki. Mwanamama Nancy López akawa huru tena akiwa na mshtuko mkubwa lakini hai.

Duarte alichukuliwa haraka na kukimbizwa kwenye gari la wagonjwa lakini tayari alikuwa ameaga dunia mara alipopigwa risasi. Lopez alikimbizwa hospitali japo alikuwa na majeraha machache tu wale mateka wawili ambao walipigwa risasi nao walipelekwa hospitali. Siku iliyofuata, López alihojiwa na waandishi wahabari kuhusu tukio lililobaki kidogo kuchukua maisha yake, alijibu, "Jana nilizaliwa upya; haikuwa siku yangu ya kufa lakini nilizaliwa upya. Namuomba Mungu ampokee (Duarte) huko juu na kumsaehe maana mambo yote haya huwa tunafanya pasipokujua kwanini tunafanya na madhara yake, wacha apumzike kwa amani na amsamehe"


Post a Comment

0 Comments