JARIBU LA USHINDI SEHEMU YA 4

 


Martin akamtajia nesi yule namba za mkewe na kisha akampigia simu na kumueleza kuwa afike hospitali ya Mt. Joseph ili kumuona mumewe.

“Asante sana nesi, unaitwa nani?” Martin alimshukuru nesi yule na kumuuliza jina lake.

“Usijali ni sadaka tu hii, naitwa Sonia” Nesi alijibu kuhu akikagua kagua chupa ya drip.

Baada ya muda daktari alifika na kusalimiana na Martin. “Unajisikiaje?” Daktari aliuliza.

“Najisikia maumivu kiasi katika kichwa, mkono na mgongo” Martin alimuelezea daktari anavyojihisi.

“Ni sawa, hata hivyo hakuna majeraha makubwa uliyopata, nimekufanyia vipimo vyote uko salama hakuna mfupa uliovunjia, uko salama na haya msumivu ni yakawaida kabisa.” Daktari alimuelezea Martin ambaye alijisikia faraja sana kusikia kuwa hakupata madhara makubwa kutokana na ajali aliyopata.

Akiwa bado anazungumza na dakari, Annabelle aliingia akiwa hana hata chembe ya shauku kutaka kujua mmewe anaendeleaje.


SASA SONGS NAYO..........

“Ooh! Mke wangu, umefika?”

“Hapana naondoka…Kwahiyo hujafa?” Annabelle aliuliza swali lililowashangaza Martin, nesi na Daktari.

“Mke wangu….” Martin alitaka kusema jambo lakini mkewe akamkatisha.

“Koma…Nabado huu ni mwanzo tu namshukuru sana Mungu kwa hili utalipia madhambi yako yote uli….” Annabelle alianza kubwatuka lakini Daktari alichoka kumvumilia.

“Hey we mama hii ni hospital siyo saluni, hebu kuwa na ustaarabu basi kama unatofauti na mumeo nenda kamsubiri nyumbani.” Nesi aling'aka, Annabelle akalielewa somo na taratiibu akaanza kuondoka kuhu akibinua mdomo. Daktari yule alibaki akimshangaa sana mke wa Martin, naye Martin alikuwa ameinamisha kichwa chske asijue nini cha kufanya.

Daktari alimgeukia Martin, “Mr. Martin, hivi huyu ni mkeo kweli?” Daktari alimuuliza Martin.

Martin alivuta pumzi na kuinua kichwa chake kumtazama Daktari huku akilazimisha tabasamu, “Doctor Rose, naomba msamaha kwa niaba ya mke wangu kuna tofauti tu za kawaida mme na mke, you know, so am….”

“It's okey haina haja ya kujieleza sana nimekuelewa, we endelea kupumzika nadhani jioni nitakuruhusu.” Daktari Rose alimueleza Martin.

“Asante sana Daktari….” 

“Ila kuwa makini na huyo mkeo maana mi sijapata kuona wanawake wa aina hii aisee kha!” 

Martin hakujibu kitu badala yake alilazimisha tabasamu ila moyoni mwake ni yeye na Mungu wake ndiyo wanajua nini kilikuwa kinaendelea katika kichwa chake na moyo wake.

“Aah! Nesi am starving naomba unisaidie kununua chakula…” Martin alimuomba nesi amsaidie kununua chakula baada ya kuhisi njaa kali.

“Sawa usijali nakuletea.” Nesi alikubali na kuanza kupiga hakuta kuondoka. 

“Subiri nikupatie hela….” Martin alianza kujipapasa ili atoe pesa lakini hakuwa na pesa yoyote.

“Martin wala usijali we tulia mi ntakununulia chakula tena kizuri sana, relax babaa”

“Aaah! Asante sana dada angu Mungu akubariki sana.” Martin alimshukuru nesi. Nesi aliondoka na kwenda kumnunulia Martin Chakula kisha akamletea. Martin alimshukuru sana nesi kwa moyo wake wa ukarimu. 

Jioni Martin aliruhusiwa na kurejea nyumbani hakumkuta mkewe alijaribu kumpigia simu lakini hakupokea. Majira ya saa 3 usiku Annabelle alirejea nyumbani na kumkuta mumewe anamsubiri. “Umetoka wapi muda huu na kwanini ulikuwa hupokei simu yako?” Martin alimuuliza mkewe.

“Ni nini unachotaka kujua zaidi?” Annabelle akimuuliza Martin huku akijitupa kwenye sofa.

“Mke wangu sikuelewi, umekuwa na tabia za ajabu ajabu, kwanini unanifanyia hivi?” Martin alilalamika lakini Annabelle hakujali hisia za mumewe alisimama na kuanza kuondoka, Martin alimzuia kwa kutumia fimbo aliyokuwa anaitumia kutembelea ili kuepusha kuumiza mguu wake wa kulia ambao ulikuwa na maumivu.

“Annabelle hatujamaliza bado, na ni nini kile ulicholifanya hospitali?”

“Martin hebu niache sawa, sina muda wakujibizana na wewe nahitaji nikapumzike…” Annabelle alimjibu Martin kisha akamsukuma akaangukia kwenye sofa, pasi na kujali kama angemuumiza mumewe au lah. Martin alitikisa kichwa na kumuomba Mungu amsaidie kuwa na moyo wa uvumilivu.

Martin hakwenda kazini kwa siku kadhaa kutokana na ajali aliyoipata hivyo aliamua kuwa na mapumziko ya siku kadhaa, hapo ndipo aliona kila aina ya rangi ambayo hakuiona. Kuna wakati alikuwa anajiuliza ‘Hivi kweli hii ndiyo aina ya mwanamke nilioa? Hivi huyu ndiye Annabelle wangu tuliyependana sana? Huyu ndiye Annabelle aliyekuwa anajali na kuumia nilipoumia, kufurahi nilipofurahi?’ Alizikumbuka zile nyakati nzuri ambazo walikuwa na furaha pamoja na binti yao, aliumia sana.

Baada ya mapumziko kuisha, Martin alirejea kazini na kuanza kazi, milango mingi ilifunguka siku hadi siku, akawa hatafuti wateja ila wateja wanamtafuta yeye.

 Siku moja akiwa amekaa na mkewe sebleni huku kila mtu akiwa na mishe zake, mara simu ya Martin ikaita. Martin akatazama katika kio cha simu yake akaona ni namba ya mtu anayemfahamu na nimuhimu sana, akaipokea, “Hallow, habari za mchana chief?” Martin alimsabahi mtu huyo aliyempigia simu. Lakini kwa kuwa kulikuwa na sauti kubwa ya television akamuomba mkewe apunguze lakuni mkewe alimpuuza ikabidi afanye hivyo yeye mwenyewe.

“Ndiyo Chief nakusikia…”

“Mr. Martin, napenda kukupa taarifa kuwa, kampuni yako imeshinda na nitakupa tutasaini mkataba kesho mchana kutekeleza mradi wa 3.2 Billions!”

“Chief are you serious? 3.2 Billion! Ooh! God Bless you, sir.”

Baada ya maongezi hayo Martin aliamua kumfikishia habari hiyo njema mkewe lakini, mkewe alinyanyuka na kusonya kisha akaingia chumbani kwake. Hilo Martin alilizoea hivyo kitendo hicho cha mkewe hakikuzuia furaha aliyokuwa nayo, aliruka ruka na kushangilia. 

Siku iliyofuata Martin alikwenda kusign mkataba wa mabilioni ya pesa. Kutokana na kazi nyingi za siku nzima, Martin alichelewa kurudi nyumbani lakini alimtaarifu mkewe kwa ujumbe mfupi wa simu kwakuwa hakupokea simu zake. Hiyo siyo mara ya kwanza kuchelewa kurudi kutokana na kazi nyingi hata hapo awali alikuwa akichelewa lakini hakuacha kuwa baba na mume mzuri kwa mtoto wao Ruth na mkewe Annabelle. Baada ya Annabelle kujua kuwa mmewe atachelewa, alikwenda kwa mlinzi na kuchukua funguo za getini ana akamueleza mlinzi asiruhusu yeyote kuingia hata kama ni Martin! 

Baada ya saa kadhaa Martin alifika, alipiga honi lakini mlinzi hakufungua, aliamua kumpigia mlinzi lakini alimueleza kuwa amepewa masharti na mama kuwa asimruhusu mtu yeyote kuingia na hata funguo amechukua! Martin alishangaa sana, akaamua kumpigia siku mkewe, lakini kama kawaida mkewe hakupokea simu. Martin aliamua kulala ndani ya gari.

Asubuhi ilipowadia, Annabelle ambaye ni mke wa Martin, alirejesha funguo kwa mlinzi hivyo Martin akaweza kufunguliwa mlango na kuingia ndani. Alikasirishwa sana na kitendo cha mkewe, alimfuata hadi chumbani kwake, “Annabelle nini maana ya hiki ulichokifanya? Yaani kwenye nyumba yangu mwenyewe, nazuiliwa kuingia, unanilaza nje kwemye gari usiku kucha, unatatizo gani wewe mwanamke?” Martin alimfokea na kumuuliza mkewe maswali mfululizo.

“Na bado nitafanya hivyo tena na tena na tena na tena kwasababu ninakuchukia sana we mwanaume hadi najuta kuolewa na wewe….!” Annabelle alimjibu Martin, majibu ambayo kamwe Martin hakuweza kuyavumilia alijikuta amenyanyua mkono wake kutaka kumpiga mkewe lakini alishangaa kuona na mkewe naye amenyanyua mkono akitaka kijibu mapigo. 

“Oooh! Na wewe pia unataka kupigana na mimi siyo?” Martin alimuuliza mkewe kana kwamba haoni kuwa mkewe kajiandaa kwa lipi.

“Jaribu uone….” Annabelle alijibu

“Huna maana…” Martin alimuacha mkewe akiwa amesimama ananesa nesa kama kafungiwa spring miguuni. Martin aliingia chumbani kwake na kujiandaa kwa ajili ya kwenda kazini. Hakumuaga mkewe aliindoka zake kimya kimya. 

Kesho yake Martin hakwenda kazini alibaki nyumbani akiwaza mambo kadha wa kadha, alitafakari ni kwa namna gani anaweza kuiokoa ndoa yake. Alisikia kuna watu wanazungumza, aliposikiliza kwa makini alisikia sauti ya rafiki wa Annabelle. Aliamka kitandani na kutoka taratibu huku akishuka ngazi kwa umakini.

“Mwenzangu yaani kila siku iendayo kwa Mungu naona hela zinajaa tu.” Annabelle alikuwa akimwambia rafiki yake aitwaye Juliet.

“Mimi nakwambia Martin ni mshirikina, utajiri wake huo siyo utajiri wa kawaida. Kwani hizo pesa anazileta humu ndani?” Juliet alimueleza Annabelle kama mumewe hutunza pesa ndani.

“Hapana, yaani kila kukicha ni simu za kupewa tenda za ujenzi ni mabilioni kwa mabilioni yaani hadi naogopa.” 

“Shoga yangu sikiliza nikwambie, ukiendelea kubaki hapa, wewe ndiye utakayefuata kamaliza mtoto anakuja kwako mama mtoto kuwa makini.” Juliet aliendelea kupigilia msumari.

Martin alishindwa kuvumilia, akaamua kujitokeza huku akipiga makofi. “Woow Juliet safi sana, kumbe wewe ndiye unamjaza maneno mke wangu unajifanya kuwa ni rafiki wa mke wangu kumbe huna lolote ila kuja kuvunja ndoa za watu.” Martin alimwambia Juliet aliyekuwa kainama kwa aibu.

“Kwani anasema uongo?” Annabelle alidakia.

“Kelele we mwanamke, mwanaume nikiongea mwanamke unatakiwa kukaa kimya.” Martin alifoka japo maneno yale hakutaka kuyatumia kumdidimiza mkewe lakini ilimbidi afanye hivyo ili kulinda ndoa yaje na heshima yake kwa mkewe pia.

“Hivi Martin….” Juliet alitaka kuongea lakini alikatishwa na sauti nzito ya yenye mamlaka ya Martin.

“Nyamaza kimya, hapa upo kwenye himaya yangu ninaweza kumufanya chochote kile na hakuna mtu hata mmoja hata marehemu babu yako akifufuka leo hataweza kunifanya chochote.” Martin alifuwa amefura kwa hasira.

Juliet aliingiwa na woga wa hali ya juu huku akiwaza juu ya habari kuwa Martin ni mshirikina, alizidi kuogopa na pia akafikiri maneno ya Martin na uwezo wa kifedha alionao, hakajuta ni kwanini alikuja hapo.

“Sasa, hivyo hivyo ulivyo, simama wima, kushoto geuka hatua tatu mbele kushoto geuka, fungua mlango utoke na usirudi tena hapa, ione hii nyumba kama kaburi. TOKA NDANI YA NYUMBA YANGU” Martin alimuamuru Juliet ambaye alitii kila alichoambiwa na Martin. Annabelle pia alikuwa ameingiwa na woga maana hakuwahi kumuona Martin akiwa amechukia namna ile. Alihisi baridi na tumbo likiunguruma kwa taratibu kama vile mtu mwenye njaa.

Baada ya Juliet kuondoka, Martin alimgeukia mkewe, “Na wewe, fanya vituko vyako vyote lakini nikikuona karibu na huyu malaya, siku hiyo utataja majina ya wanaukoo wangu wote.” Martin alimuonya mkewe kisha akarudi chumbani kwake.

 Maisha yakawa yanaendelea huku wakiwa kama chui na paka, hakuna salamu, hapaliki wala hapanyweki. Martin aliamini kuwa ipo siku lazima mambo hayo yatakwisha. Lakini alitaka zaidi kujua ni nani ambaye huwa anampa maneno namna ile hadi anazidi kuwa mtu wa ajabu kila kukucha, kila alipowaza hakupata jibu, aliendelea kumuomba Mungu mambo yaishe mapema maana amemkumbuka sana mke halisi.

Ilifika siku ya kusherehekea miaka 15 ya ndoa yao lakini pia ilikuwa ni kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa ya Annabelle. Martin aliamua kumnunulia mkewe zawadi kumpongeza kwa siku yake ya kuzaliwa lakini pia kumshukuru kwa kuwa naye hadi wakati huo japo kuwa alikuwa anamfanyia vitu visivyo stahili, bado alibaki kuwa mke wa thamani sana kwake na ndiyo maana alimvumilia kwa kila bala alilomtendea.

Itaendelea...........


USIKOSE SEHEMU YA 5 YA HADITHI HII KESHO

Post a Comment

0 Comments