NA GEOFREY DISMAS
Tatizo la akili si tatizo
dogo hasa kwa watu maarufu wakiwemo waigizaji, wanamichezo na wanamuziki. Kila
aliyefanikiwa katika tasnia hizo, aliwahi kupitia changamoto ya tatizo la akili
na wengine walishindwa vita hiyo wakapoteza na wengine hawakupoteza, walishinda.
Wapo waliotoka hadharani na kuelezea namna walivyokutana na changamoto hiyo
lakini wapo ambao hadi leo hawakuwahi kujitokeza hadharani na wengine
walipoteza maisha kwa kutumia dawa za kulevya na wengine walijiua kwakukosa
msaada.
Kila mtu maarufu na mwenye mafanikio aliwahi kupitia changamoto hii ya tatizo la akili wafuatao ni baadhi ya wasanii na wanamichezo waliowahi kupitia changamoto hii;
![]() |
Amanda Byenes |
AMANDA
BYENES
Muigizaji Amanda Bynes, Mnamo mwaka wa 2014, nyota huyo wa Easy A aliwekwa kwenye kituo maaluu cha kutibu watu wenye matatizo ya akili ambapo huko alikaa kwa takribani miaka 9 akitibiwa baada ya kugunduliwa na ugonjwa unaotambulika kama Bipolar Affective Disorder and Manic Depression kwa tafsiri isiyo rasmi tunaweza kuuita ugonjwa wa hisia na unyogovu wa kihemko. Hatua hiyo ilichukuliwa baada ya Bynes kukutwa mitaa ya jiji la LA akiwa uchi. Mnamo Machi 2022, Bynes aliachiliwa kutoka kwenye kituo hicho ambako alikaa kwa miaka 9 chini ya uangalizi wa wataalamu na wazazi wake.
![]() |
Ryan Reynolds |
RYAN
REYNOLDS
Muigizaji huyo mwenye
umri wa miaka 45 amekabiliana na tatizo la kuwa na wasiwasi mkubwa tangu akiwa
mtoto, Reynolds alisema kwenye kituo cha TV kiitwacho CBS.
"Nimekuwa na tatizo
la kuwa na wasiwasi maisha yangu yote kwa kweli. Na unajua, ninahisi kama nina
sehemu mbili za maisha yangu, ambayo moja inachukua nafasi hiyo
inapotokea," Reynolds alisema.
Reynold anaongeza kwa kusema watu wanavyomtazama kwenye TV ni tofauti na maisha yake akiwa nje ya TV.
![]() |
Britney Spears |
BRITNEY
SPEARS
Mwanamuziki maarufu kutoka nchini marekani Britney Spears aliwahi kukiri waziwazi kuhusu tatizo lake la akili kupitia mtandao wake wa kijamii. Tatizo lake la akili linatokana na wale waliowahi kumuumiza katika maisha yake na hata mitandao ya kijamii. Watu wa karibu na mwanamuziki huyu waliwahi kukaririwa wakisema Spears anaonekana kukata tamaa kabisa. Katika mtandao wa kijamii wa Instagram kupitia akaunti yake aliwahi kusema kuwa maisha ya mastaa kwenye mitandao ya kijamii siyo maisha halisi.
![]() |
Aaron Carter |
AARON
CARTER
Mwimbaji Aaron Carter
ambaye sasa ni marehemu, alifichua kuwa anapambana na matatizo mengi ya afya ya
akili, multiple personality disorder, schizophrenia, acute anxiety na manic
depression katika kipindi cha The Doctors. Carter ambaye wakati huo alikuwa na
miaka 31, alijulikana sana kama nyota wa muziki wa pop tangu akiwa mdogo, katika
kipindi hicho aliorodhesha takribani dawa sita ambazo anatibiwa nazo.
"Huu ndio ukweli
wangu," Carter alisema huku akiinua mfuko wa plastiki wa chupa nyingi za
dawa kwenye klipu moja iliyotrend sana wakati huo katika mtandao wa facebook.
Carter pia aliwahi
mpeleka mama yake mzazi Jane, kwenye onyesho, na kuwaomba waandaaji waandaaji
Dr. Travis Stork na Dk. Judy Ho wamsaidie mama yake aachane na matumizi ya
pombe ya kupindukia kwani alikuwa anahofu kuwa mama yake anaweza kujikuta
katika hali mbaya Zaidi.
Carter alifariki novemba
25 mwaka jana akiwa na miaka 34. Mwili wake ulikutwa bafuni na msaidizi wake wa
nyumbani huko Lancaster, California nchini marekani huku chanzo cha kifo
kikitajwa ni kuzidisha dawa za kulevya.
![]() |
Howie Mandel |
HOWIE
MANDEL
Howie Mandel kwa muda
mrefu amekuwa wazi kuhusu matatizo ya kiafya ambayo ameshughulika nayo kwa
miaka mingi - linapokuja suala la maradhi ya mwili na shida za afya ya akili
Mandel amekuwa mstari wa mbele kabisa kupambana.
Jaji huyu maarufu kutoka
katika shindano maarufu la America's Got Talent, ambaye anapambana kwa muda mrefu na matatizo ya akili na msongo
wa mawazo kama vile Obsessive Compulsive Disorder (OCD) na Attention Deficient
Hyperactivity Disorder (ADHD) ni wakili mzuri wa kukomesha unyanyapaa unaowakabili
wagonjwa wa matatizo haya ya akili.
"Tunatunza afya yetu
ya meno, hatujali afya yetu ya akili." Alimwambia Jay Leno mwaka wa 2014
Alidai kuwa unyanyapaa na
ukimya kuhusu afya ya akili unatokana na ukosefu wa elimu katika jamii ya
wamarekani.
"Tuko nyuma sana
ulimwenguni kiasi cha kutokuwa na shule mahali ambacho inafundisha kila mtu
jinsi ya kutambua na kuikubali hali hii,"aliongeza. "Nadhani
suluhisho la kufanya ulimwengu huu kuwa bora ni ikiwa tungekuwa na afya njema,
kiakili." Alimalizia.
![]() |
Naomi Osaka |
NAOMI
OSAKA
Jina hili siyo geni kwa
wapenzi wa tenesi duniani. Nyota huyu wa mchezo wa tenesi tayari ameonja tamu
na chungu ya kuwa maarufu.
Osaka aligeuka kuwa nyota
akiwa na miaka 15 tu. Osaka katika maisha yake ya kuwa mcheza tenesi nyota
amekwisha nyakua mataji manne ya Grand Slam na kuorodheshwa kama mchezaji namba
moja bora wa tenisi na Chama cha Tenisi cha Wanawake duniani. Mnamo 2020, alishinda
tuzo ya Associated Press kama Mwanariadha bora wa Kike wa Mwaka.
Lakini nyota huyo wa Marekani
mwenye asili ya Kijapani ambaye sasa ana miaka 25, amekuwa akikabiliana na
wasiwasi na mfadhaiko kwa muda mrefu. Masuala haya ya afya ya akili yameathiri
uwezo wake wa kutekeleza majukumu yake ya kikazi, kama vile kushiriki katika
mikutano ya wanahabari na vyombo vya habari. Wakati Osaka anafanya maamuzi ya
kujiondoa kwa hiyari kwenye mashindano ya French Open ya mwaka 2021 ili kuipa
kipaumbele afya yake ya akili, alipokea upinzani kutoka kwa vyombo vya habari
hasa pale alipokwepa kufanya mazungumzo na wanahabari.
"Kunaweza kuwa na
wakati kwa yeyote kati yetu ambapo tunashughulikia masuala fulani nyuma ya pazia,"
Osaka aliandika kwenye TIMEs. "Kila mmoja wetu kama wanadamu anapitia kitu
kwa kiwango fulani." Aliongeza.
Osaka alikuwa
anasumbuliwa na matatizo ya afya ya akili tangu mwaka 2018 katika mashindano ya
US Open. Alipigwa faini ya Dola 15,000 za marekani kwa kukwepa mkutano na
wanahabari.
SERENA
WILLIAMS
Hakuna asiyemfahamu nyota
huyu na legendary katika mchezo wa tenesi na mwanaharakati wa masuala
mbalimbali. Kuhusu suala la afya ya akili yeye anasema huwa anaweka mipaka
mikari au madhubuti hasa linapokuja suala kama hilo la afya ya akili. Serena
alisema hayo akiwa katika video call na Popstar na muigizaji kutoka katika
kiwanda cha filamu cha Hollywood.
Serena alisema yeye
hupanga muda wa kujifanyia tathmini ya afya ya akili ili asije kufikia katika
hali mbaya. Serena amenyakuwa Grand Slam 23 katika wakati wote ambao amekuwa
active katika mchezo wa tenesi.
![]() |
Michael Phelps |
MICHAEL
PHELPS
Kila siku Michael Phelps
hufanya mazoezi katika gym iliyopo nyumbani kwake kuweka mwili wake sawa lakini
huwa hasahau kamwe kushughulikia afya yake ya akili kila siku. Phelps ni
mshindi wa Olympic wa mchezo wa kuogelea wa Marekani wa muda wote
“Katika kipindi chote cha
kucheza mchezo huu, nimekuwa nikizungukwa na timu ya watu ambao kazi yao
nikuhakikisha nakuwa bora kimwili. Kama nahitaji kuwa imara, kuna kuwa na watu
10 ambao kazi yao ni kutafuta njia za kunifanya nakuwa imara sana. Lakini
linapokuja suala la akili, hakuna mtu hata mmoja” Phelps aliuambia mtanao wa
Healthline.
Baada ya kuishi na msongo
wa mawazo, hofu, na mawazo ya kujiua kwa miaka kadhaa, aliamua kuweka
kipaumbele katika afya ya mwili na akili yake.
Mwaka 2004, baada ya
kushinda medali 6 za dhahabu na 2 za shaba katika mashindano ya Athens
Olympics, Phelps anasema alianza kuhisi msongo wa mawazo wa baada ya ushindi (post-Olympic
depression)
“Unajibidiisha kwa miaka
4 ili kufikia katika hatua hiyo, halafu unafika katika hatua hiyo uliyoitamani
sana…Juu kabisa ya kilele cha mlima, halafu unajiuliza sasa natakiwa kufanya
nini baada ya hapa? Natakiwa kwenda wapi? Mimi ni nani?” Alisema.
Aliamua kuchukua
mapumziko mafupi, lakini akarudi tena katika mazoezi muda mfupi mwaka 2004
baada ya mashindano ya Olympics kutamatika, akaenda kushindana kwenye Olympic
ya mwaka 2008 na 2012.
Phelps aliendelea
kutaabika na kujitenga na wenzake, kujifungia chumbani kwa muda mrefu “Kisha
nikaamua ni muda sasa wa kuchukua hatua kutafuta mkondo mwingine, njia tofauti”
alisema.
Mwaka 2014, baada ya kukubali
kuwa anahitaji msaada,Phelps aliamua kwenda katika kituo cha kusaidia watu
wenye uhitaji wa matatizo ya akili ambako huko alikaa kwa siku 45 akipatiwa
matibabu.
“Mara baada ya kutoka nje,
niliendelea na matibabu (therapy) ambayo niliyapata kwenye kile kituo
nilichokuwa natibiwa. Kwangu mimi, unajua, wakati naanza niliona ni kitu cha
kutisha, kitu cha kuogofya, kitu ambacho ni kipya na sikujua namna ya kukipokea,
na nadhani hapo nipo udhaifu wangu ulipojitokeza kwa mara ya kwanza.” Alisema Phelps.
Phelps anasema baada ya
kutoka katika kituo alichokuwa anapatiwa matibabu alijihisi amepona kabisa tatizo
la afya ya akili na kwamba yuko tayari kwa kazi. Anaendelea kwa kusema alianza
kujitambua yeye ni nani na mwenye jukumu gani na si tu ni binadamu bali pia ni
mwogeleaji ambayo ndiyo kazi yake.
![]() |
Chloe Kim |
CHLOE
KIM
Mapema mwaka jana wa
2022, binti wa miaka 22, mmoja wa washindi wa Olympic katika mchezo wa kuteleza
kwenye barafu na mshindi wa medali ya dhahabu, Chloe Kim alitangaza kuwa atakaa
nje ya michezo kujipa mapumziko ili ajikite katika kushughulikia afya yake ya
akili. Katika mkutano wa 2022 wa Teen Vogue Summit uliofanyika huko Los
Angeles, alifunguka kuhusu uamuzi wake huo.
“Nimetambua katika
Olympics yangu ya kwanza yam waka 2016, nilichukia mchezo wa kuteleza kwenye
barafu,” alisema na kuongeza, “Sikuhitaji kufanya tena kabisa, na sikuwa mawazo
ya kurudi kabisa huko…Niliamua kwenda shule kwa muda, na niliona ni kwa namna
gani ilivyo na manufaa sana kwangu. Hivyo baada ya kurudi kutoka Beijing kwenye
Olympics yangu ya pili, niliona ninahitaji kupumzika kidogo kwa sababu
nilipoteza kabisa yale mapenzi yangu na mchezo huo.”
Chloe aliunga mkono hoja
ya mshindi wa medali ya dhahabu katika Olympic, Simone Biles ambaye alisema
kuweka kipaombele katika afya ya akili kwa mwanamichezo ni jambo la lazima. Katika maelezo yake Chloe anasema sababu
nyingine iliyompelekea katika hali hiyo, ni kutokana na kukosa uhuru wa kufanya
baadhi ya vitu mara baada ya kuwa maarufu. Anasema mara baada ya kushinda
medali ya dhahabu hakuweza kwenda katika migahawa aliyozoea kwenda, hakuweza
kwenda katika sehemu alizozoea kwenda. Hali hiyo imfanya achukie medali ya
dhahabu aliyo shinda na aliichukua pamoja na vifaa vyake vya kutelezea kwenye barafu
akavitupa kwenye chombo cha takataka.
Kwa
kuhitimisha, Kwa mujibu wa shirika la afya duniani
kwenye ripoti yao yam waka 2019, walieleza kuwa mtu 1 kati ya watu 8, au watu milioni
970 duniani kote wanasumbuliwa na matatizo ya akili ikiwemo woga mkubwa au
anxiety na unyongovu au depressive disorders.
Afya ya akili haiwaathiri
tu watu maarufu japo kuwa wao wapo kwenye hatari zaidi lakini kila mtu anaweza
kukumbwa na ugonywa huu wa afya ya akili. Kwa nchi nyingi za kiafrika hasa
Tanzania bado uelewa ni mdogo sana miongoni mwa jamii, ni wito wangu kwa
serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali, taasisi za dini pamoja na viongozi wa
kimila kuona umuhimu wa kuitambua uwepo wa tatizo hili la afya ya akili na
kuchukua hatua muhimu na kuweka nguvu kukabiliana nalo angali halijawa kubwa
kwani likiwa kubwa udhibiti wake utakuwa wa gharama kubwa sana.
0 Comments