JARIBU LA USHINDI SEHEMU YA 6

 



ILIPOISHIA.............

Stanley alitulia kidogo na kuvuta pumzi ndefu kisha kuitoa nje. Alijitengeneza vyema kwenye sofa lenye gharama ya kununua pikipiki aina ya Boxer kadhaa hivi.

“Uncle, pesa ninayo ya kutosha nikimaliza nitakwambia.” Akijibu Stanley.

“Sasa kumbe shida nini? Hebu funguka basi au kam hutaki useme.” Kiasi fulani sauti ya mjomba wake ilionesha kukereka kutokana na kucheleweshwa kupatiwa habari aliyo ihitaji.

“uncle unakumbuka siku nakwenda kutumikia jamii nilikupigia simu nikakwambia kuna tukio lilitokea na nikakwambia nitakueleza nikirudi?” Stanley alianza kufunguka.


SASA SONGA NAYO.............

“Ndiyo! Kwahiyo unabadili mada au ni ile ile?” Mjomba wake aliuliza huku akijiandaa kuendelea kusoma gazeti lake akijua wazi kuwa ni kawaida ya Stanley kuanzisha mada mpya kila unapombana akueleze juu ya kinachomsibu. Stanley hakuwa mtu wakushirikisha mtu mwingine juu ya matatizo yake, hupenda kupambana mwenyewe hadi atakaposhindwa kabisa ndipo aombe msaada, hivyo hakushangaa alijua fika kuwa hakuna kilichobadilika kwa kijana huyo, lakini siku hiyo ilikuwa tofauti.

“Hapana mjomba, wala sibadili mada…...Siku ile nimetoka hapa nilienda hadi stendi na nikapanda bus nikashuka njiani ili nipande gari za kwenda kijijini. Lakini dakika kadhaa baada ya kushuka, walitokea wanaume wawili wakiwa wamejifunika nyuso huku wakiwa na bastola, walinipora kila kitu na kunibakishia kitambulisho cha uraia tu!” Stanley alimuelezea mjomba wake kwa masikitiko.

“Mmh! Sasa mbona hukunieleza badala yake ukanieleza mambo tofauti” Mjomba wake alimshangaa kwa kuwa alikuwa kimya. Stanley hakujibu kitu, alitulia kama mtu aliyevuta taswira ya jambo fulani, akatikisa kichwa kusikitika kisha akaendelea, “Hiyo ni cha mtoto, nikijaribu kuomba msaada lakini hakuna ambaye alinisaidia. Gari kwenda kijijini zote hazikujubali kunichukua kwakuwa sikuwa na pesa, hata wale wenye gari binafsi nao walikataa kunichukua.” 

“Pole sana uncle, sasa usiwe mnyonge hivyo uko salama nyumbani au unahitaji msaada wa mtaalamu wa Psychology?” Mjomba wake Stanley alimuuliza.

“Hapana uncle!” Alijibu Stanley.

“Nini sasa kinakufanya uwe hivyo, unanitisha.” Mjomba wake alimuuliza huku akimchunguza kwa makini.

“Bado story inaendelea….” Alijibu Stanley huku akijiweka vyema katika kiti.

“Niliendelea kuwa na subra na hadi nilipoona gari aina ya Land cruiser VX niaisimamisha. Alikuwa ni familia ya mume, mke na mtoto wao wa kike. Nilimsalimu na kumueleza yaliyonisibu, hakuniamini moja kwa moja nikamuonesha kitambulisho akasoma jina  langu kisha akashauriana na mkewe na wakanikubalia nipande ndani ya gari yao.” Stanley aliendelea kumuekeza mjomba wake.

“Dah!” mjomba wake alishangaa kidogo 

“Lakini tukiwa njiani tulivamiwa na wanaume kadhaa wakiwa na silaha la moto, wakituamuru kushuka kutoka garini, tulitii. Wakasema wanahitaji mtu kwa ajili ya kafara !” Stanley alisimulia huku machozi yakimlenga lenga. 

“Wait, umesema kafala?” Mjomba wake alishangaa kusikia hivyo.

“Ndiyo ni kafala…” Akijibu Stanley huku naye akimshangaa mjomba wake alivyoshangaa. 

 

Stanley aliendelea kumsimulia Mjomba wake, “Yule baba aliyenipa lift aliwasihi asiumize familia yake na angekuwa tayari kuwapa kiasi chochote cha fedha ili wasituumize!” Alisita kidogo kusimulia kisha akaendelea, tayari machozi yalikuwa yameanza kutiririka shavuni. 

“Watu wale walikataa wakasema wanahitaji kichwa cha mtu, yule baba alijitoa yeye ndiyo atumike katika kafara hiyo lakini watu wale walikataa na waksema wanataka kijana kati ya mimi au binti yake……Lakini cha ajabu baba yule aliamua kumtoa mwanaye wa pekee na binti yake mpendwa ili mimi nipone, ilinishangaza sana. Walinchukua binti yule na kuondoka naye, baba yule alipiga magoti na kulia sana huku mkewe akimlamu kwa kitendo alichokifanya.!” Sasa Stanley alikuwa anafuta machozi.

“Mmh! Maajabu haya, hadi leo kuna watu wenye moyo wa namna hii kweli katika hii dunia? Yaani alimtoa binti yake kuokoa maisha ya stranger?” Mjomba wake alishangaa sana. Kilichomshangaza siyo watu kutoa kafara ya binadamu ili kupata jambo fulani, bali ni moyo wa mtu huyo kukubali kumtoa mwanaye wa pekee ili kuokoa maisha ya kijana mwingine ambaye kakutana naye tu barabarani. Kwa akili ya haraka haraka ya kibinafai sana angeweza kuruhusu wamchukue kijana huyo ili familia yake iwe salama lakini badala yake kwanza alijitoa yeye ili familia yake na kijana huyo ambaye kwa wakati huo ilikuwa ni jukumu lake na iliposhindikana ikabidi amtoe binti yake! Ilimshangaza sana.

“Kwahiyo huyo jamaa unamfahamu kwa jina au mahali anapoishi au ulichukua namba zake?” Mjomba wake alimuuliza.

“Hapana uncle na hicho ndicho kinaniumiza sana” Alijibu Stanley kinyonge sana.

“Dah! Angalau ungekuwa unamjua jina au mahali anapoishi tungeweza kumtafuta, binti yake hakukutajia jina lake?” Mjomba we alimuuliza tena.

“Hapana pamoja na maongezi yote tulipokuwa safarini, sijufikiria kumuuliza jina lake.” 

“Stanley, pole sana tuiombee hiyo familia naamini inapitia wakati mgumu sana.” Mjomba wake alimweleza Stanley ambaye aliitikia kwa kichwa huku akifuta machozi.

Baada ya wiki moja kupita Mke wa Stanley alianza kuyazoea maisha ya bila mumewe, alikuwa anajihisi ni kama mtu aliyetua mzigo mzito aliokuwa ameubeba kwa muda mrefu kutoka safari ya mbali. Mama yake alikuwa upande wake siku zote kitendo ambacho kingeweza kufanywa na mzazi yeyote katika zama hizi. Annabelle akiwa amekaa na mama yake, walisikia mlango ukigongwa, mdogo wake Annabelle aitwaye Dan alienda kufungua mlango, mgeni hakuwa mtu mwingine bali ni mtu aliyezoea kumuona mara kwa mara, Martin!

“Karibu shemeji, shikamoo” Dan alimsalimu Martin bila kinyongo hadi Martin nwenyewe alishangaa.

“Asante, mama nimemkuta?” Martin aliuliza akiwa bado kasimama nje.

“Ndiyo wapo, pita ndani tafadhali.” Dan alimkaribisha tena shemeji yake.

 

Martin aliingia ndani huku akiwa ni mtu asiyejiamini sana, mara akakutana na macho ya mama mkwe wake! Ni kama moyo wa Martin uhamie kulia kwa namna alivyostuka.

“Umefuata nini hapa?” Ndiyo sentensi pekee iliyotoka kinywani mwa Mama Annabelle.

“Shikamoo mama….” Martin msalimu mama mkwe wake lakini bado mfululizo wa majibu ya kukatisha tamaa na maswali ya kuashiria kuwa ‘huhitajiki hapa' yaliendelea.

“Mama sijaja kwa shari nimekuja kuzungumza na wewe pamoja na mke….” Kabla hajamaliza kuongea alikatishwa na Annabelle.

“Ishia hapo hapo, mimi siyo mkeo.” Alijibu Annabelle kwa hasira.

“Najua unahasira na mimi lakini nawaomba mnielewe mimi sijamtoa kafara mtoto wangu ili nipate mali.” Martin aliendeleza ushawishi lakini ni kama kumpigia mbuzi ngoma acheze.

“Ooh! Kwahiyo binti yangu yuko wapi?” Annabelle alikamuuliza huku amemshikia kiuno.

“Hamuwezi nielewa lakin….”

“Kweli kabisa hatuwezi kukuelewa wala kuku wa mayai, naomba uondoe kongoro zako hapa na usithubutu kurudi tena hapa…. Toka ndani kwangu mshirikina mkubwa wewe, unataka unimalizie na mwanangu?” Mama Annabelle alifoka. 

Martin akiona kuwa kwa hali ilivyo hapo, asiwengeza kusikilizwa badala yake angeishia kuitiwa polisi au kuumizwa, ilimbidi atii na kuondoka zake.

Stanley mpwa wa Mr. Jerome alikwenda katika hospitali moja ya serikali ambako rafiki yake wayesoma wote kozi ya udaktari alikuwa anajitolea katika hospitali hiyo. Lengo likikuwa kuchukua kitabu chake ambacho alimuazima rafiki yake huyo aitwaye Rahma. Walikutana katika chumba cha wagonjwa wa dharula, walisalimiana kisha Stanley akamuekeza kusudi la yeye kuja hapo.

“Ooh! Samahani sana best nimekisahau tena nyumbani…” Rahma alimueleza Stanley maelezo ambayo yalimfanya anyong'onyee sana kwani alikuwa anakihitaji sana kitabu hicho.

“Dah! Umenikata moto kabisa mama angu” 

“Usiwaze, leo natoka mapema, nitakuletea nyumbani” Rahma alimuondoa wasiwasi.

“Hapo utakuwa umefanya la mbolea sana.”

Wakiwa katikati ya maongezi, Stanley aliona binti mmoja anakokota na manesi wawili huku macho yake akiwa kayafumba. Stanley alihisi kama aliwahi kumuona mahali na ni kama anamfananisha. Alipata shauku ya kwenda kumtazama kwa makini ili ahakikishe kuwa ni yeye. Naam hakuwa mbali na kile alichokifikiria, alimtambua binti huyo alipomsogelea karibu, hakuamini macho yake, aliinua mikono yake juu na kumshukuru MUNGU. Wauguzi walinahangaa kisha wakaendelea na jukumu lao la kumpeleka binti huyo walipokuwa wamekusudia kabla ya kusimamishwa na Stanley.

“Hey, vipi unamfahamu huyo binti?” Rahma aliuliza.

“Ndiyo namfahamu, yuko hapa kwa muda gani na nini kilimpata?” Stanley alimuuliza Rahma.

“Anamiezi kama sita sasa aliletwa hapa akiwa hoi alipata ajali ya gari na ni yeye tu ndiye aliyenusurika…. Kwani unamfahamu vipi huyu binti?” Rahma alimjibu Stanley na kisha kumuuliza swali. Swali ambalo halikujibiwa, badala yake alimwambia “Asante” kisha akamkumbusha kuhusu kitabu, baada ya hapo Stanley aliondoka mbio hadi nyumbani anakoishi na mjomba wake.

Alipofika nyumbani, Stanley hakumkuta mjomba wake, alisahau kuwa yuko ofisini kwake. Akimpigia simu na kumuomba amrusuhu kuongea na yeye ofisini kwake. Mjomba wake alimruhusu, Stanley akaondoka na kuelekea ofisini kwa mjomba wake. Alifika baada ya nusu saa kwakuwa alikuwa anatumia gani binafsi aliyopewa na Njomba we siku ya sherehe yake ya kuzaliwa. Afika ofisini kwa mjomba wake. “Nimemwona” Ndilo neno alilolisema mara tu aliposimama mbele ya mjomb wake.

“Umemuona nani?” Mjomba wake aliuliza.

“Nimemuona yule binti ambaye nilikusimulia wati ule kuhusu baba yake kuruhusu achukuliwe ili mimi nipone.!” Alijibu Stanley.

“Una hakika ni yeye?” Mjomba wake alimuuliza huku naye akiwa na mshangao.

“Uncle ni yeye kabisa….Yupo hospitali ya Obasanjo mtaa wa Lua!” Alijibu.

“Hebu nipeleke!” Mjomba wake alimwambia na wakatoka wote ofisini. Waliingia ndani ya gari na kuondoka pamoja kuelekea Lua Street ambako inapatikana hospitali ya Obasanjo. Ni mwendo wa nusu saa toka ofisini kwa Mr. Jerome kwa kuwa kulikuwa na foleni kubwa, wakati ambapo hakuna foleni huwa ni mwendo wa dakika 15 tu.

Baada ya Nusu saa walifika na kuegesha gari zao yao katika eneo la maegesho ya hospitali hiyo. Walishuka na kuelekea moja kwa moja mapokezi, walitoa maelezo ya mtu wanayemtafuta na kwakuwa mgonjwa waliyekuwa wanamuulizia kwa mujibu wa maelezo yao katika hospitali hiyo alikuwa peke yake. Muuguzi aliyekuwa mapokezi aliwaelekeza kwenda kuonana na daktari anayemhudumia mgonjwa huyo.

Hawakupoteza muda, moja kwa moja walielekea katika chumba cha daktari walichoelekezwa, walifika na kuingia tu pila kugonga hali iliyomstua daktari huyo.

“Mzee vipi mbona unaingia kwa fujo namna hiyo nini tatizo……” Aliwauliza kwa kufoka.

“Samahani sana Daktari……Ni kama nakufananisha, wewe siyo Ogbona Ikechuku?” Mjomba we Stanley alimuuliza Daktari aliyesimama mbele yake.

“Jerome Edochie! Kha! Umenenepa hivi rafiki yangu unakula vitu gani bwana?” Daktari naye hasira ziliisha baada ya kumtazama aliyeko mbele yake, alikuwa ni rafiki yake waliyesoma pamoja sekondari kisha wakapotezana baada ya kila mmoja kwenda A-Level. 


Itaendelea............

Post a Comment

0 Comments