JARIBU LA USHINDI SEHEMU YA 5

 

 



ILIPOISHIA..........

Maisha yakawa yanaendelea huku wakiwa kama chui na paka, hakuna salamu, hapaliki wala hapanyweki. Martin aliamini kuwa ipo siku lazima mambo hayo yatakwisha. Lakini alitaka zaidi kujua ni nani ambaye huwa anampa maneno namna ile hadi anazidi kuwa mtu wa ajabu kila kukucha, kila alipowaza hakupata jibu, aliendelea kumuomba Mungu mambo yaishe mapema maana amemkumbuka sana mke halisi.

Ilifika siku ya kusherehekea miaka 15 ya ndoa yao lakini pia ilikuwa ni kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa ya Annabelle. Martin aliamua kumnunulia mkewe zawadi kumpongeza kwa siku yake ya kuzaliwa lakini pia kumshukuru kwa kuwa naye hadi wakati huo japo kuwa alikuwa anamfanyia vitu visivyo stahili, bado alibaki kuwa mke wa thamani sana kwake na ndiyo maana alimvumilia kwa kila bala alilomtendea.


SASA ENDELEA..........

Aliwahi kurudi siku hiyo hadi mke wake akashangaa ni kwanini amewahi kurudi namna ile. “Umewahi kurudi mapema hivi kuna nini?” Annabelle alimuuliza Martin aliyekuwa akimimina mafundo kadhaa ya maji.

Martin alimtazama mkewe kisha akatabasamu, “kumbe kuna wakati unajali kuhusu mimi!”

“Sijali chochote nimeuliza tu ili kama kuna mtu anataka kukuua nimpe ushirikiano.” Annabelle alimjibu mumewe huku akimimina mvinyo kwenye glass na kuumiminia wote kinywani.

Baada ya dakika chache kupita, simu ya Martin iliita mkewe akiwa chumbani kwake. Aliipokea, “Hallow boss, tayari ule mzigo uko hapa” Ilisikika sauti ya mpigaji wa simu.

“Okey, ulishauingiza ndani?” Martin alimuuliza yule mpigaji wa simu.

“Bado niko nje kabisa boss”

“Sawa, nampa maelekezo mlinzi hapo atakufungulia geti, uuweke huo mzigo hapo Karibu na huo mti mzuri hapo.”

“Sawa boss.”

Martin alimpigia mlinzi na kumpa maelekezo ambayo aliyafuata kama alivyoelekezwa.

Martin alikaa kwa dakika kama 10 kisha akaenda chumbani kwa mkewe kumuamsha.

“Nini wewe unanisumbua mimi nimepumzika, hebu niache huko”

“Tafadhali mke wangu naomba uongozane na mimi nina kitu cha kukuonesha.” Martin alimsisitiza sana mkewe.

“Kitu gani?” Aliuliza Annabelle. 

“Tafadhali we nifuate mke wangu.” 

Annabelle alikubali kumfuata Martin pengine siku hiyo majini yake yalikuwa yamelala maana alikuwa mpole sana. Walipofika nje, Martin alimtazama mkewe kisha akamwambia, “Surprise mke wangu, leo ni kumbukumbu siku ya kuzaliwa kwako nimekupa zawadi ya gari ambayo umekuwa ukiitaka siku zote na nilikuahidi kukupatia, Range Rover na ile chupa ya Champaign pale, ni kwa ajili ya kusherehekea miaka 15 ya ndoa yetu…. Happy Birthday to you honey and Happy anniversary to us!”

Baada ya Martin kuongea Annabelle aligeuka na kurudi ndani. Martin alibaki akishangaa kuona mkewe hajafurahia, aliamua kumfuata ndani ili kujua sababu ya kwanini ameondoka bila kusema chochote.

Alifika na kumkuta mkewe ana zunguka zunguka chumbani huku akionekana kuwa mwenye hasira sana.

“Baby What’s wrong with you, umeondoka kwa hasira tu nini tatizo?” Martin alimuuliza mkewe ambaye baada ya kumuona mumewe anaingia chumbani, akasimama akimtazama kana kwamba alikuwa akimsubiria kwa hamu. 

“Ulitegemea nini labda?”  Annabelle aliuliza kwa hasira.

“Mke wangu mpenzi nimekununulia zawadi ya kukupongeza kwa kuongeza mwaka mwingine na pia kukupongeza kwa kuwa umekuwa mke bora kwangu kwa miaka….” 

“Sikiliza Martin sitaki hizo ngonjela zako, umemuua mwanangu ili upate utajiri. Hongera umefanikiwa lakini nikwambie jambo moja, sitashiriki katika kutumia pesa haramu, pesa za kishirikina ambazo umezipata kwa kumuua mwanangu.” Annabelle aliongea kwa uchungu huku machozi yakimtoka.

“Annabelle unasemaje?” Martin alimuuliza tena mkewe kana kwamba hakuwa amemsikia vyema.

“Ndiyo wewe ni muuaji, utajiri wako wote umejaa damu zatu, umekanyaga maiti za watu wengi ili upate utajiri huu, najuta kuolewa na wewe Muuaji mkubwa.” Annabelle alikuwa amefura kwa hasira lakini hakujua kuwa Martin alikuwa na hasira na uchungu zaidi yake. Alipomaliza kuongea alisikia kibao kikali kikipenya katika shavu lake la kulia. Annabelle alihisi kama anaona giza kisha mwanga halafu giza kisha mwanga, alihisi sikio lake likipata moto.

“Martin unathubutu kunipiga!” Annabelle alilalamika kwa mshangao. Hakutarajia kupigwa kibao hicho.

Martin akizinduka kama mtu aliyekuwa katika ulimwengu mwingibe kabisa. Akijutia uamuzi wake wakumpiga kibao mke wake kipenzi. Alijutia kushindwa kujizuia na kuruhusu hasira zake zimtawale.

“Mpenzi Samahani….” Martin akimuomba msamaha mkewe huku akipa magoti.

“Ondoka chumbani kwangu Martin sasa hivi ondokaaaa”

“Mke wangu Annabelle samahani nimekosea naomba unisamehe.” Martin aliendelea kumuomba msamaha mkewe huku akiwa amepiga magoti chini.

“Nasema tokaaaaaaaa!” Annabelle alipandisha sauti yake juu iliyomfanya Martin atii amri ya mkewe.

Martin alijilaumu sana kwa kitendo kile. Tangu ameona na mkewe, hajawahi kumpiga kabisa, kitendo kile kilimfadhaisha sana. Alitoka ndani ya chumba cha mkewe na kwenda kukaa Sebuleni. Alimsikia mkewe akilia sana lakini kurudi chumbani kwa mkewe haikuwa chaguo bora, aliamua kutulia.

Annabelle alimpigia simu mama yake na kumlalamikia kuwa amepigwa na Martin! Mama yake Annabelle hakutaka kuvumilia kabisa, aliamua kuwapigia simu Baba zake wakubwa na wadogo wa Martin na kuwaeleza nia yake ya kwenda kumchukua binti yake. Hsikuwa habar njema kwao, waliamua kumshauri mama yake Annabelle asifanye hivyo badala yake waende wote kutatua suala hilo. Mama yake Annabelle alikubali ombi la ndugu wa Martin. 

Siku iliwadia, kikao cha wanafamilia kiliandaliwa nyumbani kwa Martin. Baba zake wadogo wawili, baba yake mkubwa mmoja na wazee wa kimila wawili. Upande wa Annabelle akiwakilishwa na mama yake tu. Mama yake Annabelle alikuwa ni mtu wa shari sana katika kikao kile aliweza kuwamudu vyema upande wa Martin, uamuzi wake ulikuwa ni kuondoka na binti yake. Baba zake wadogo na Martin wakiamua kufanya kazi ya ziada ili kuhakikisha mama huyo anatulia, walifanikiwa kuntuliza mama Annabelle. 

“Mama Annabelle tunaelewa namna unavyojisikia lakini hebu kuwa mvumilivu, lengo la kikao hiki siyo kuebdeleza ugomvi bali dhumuni ni kusuluhisha ugomvi wa watoto wetu ili amani na furaha irejee kama awali.” Mmoja wa baba zake wadogo Martin alimueleza na kumsihi mama Annabelle apunguze munkali.

“Kwa heshima yako nitatulia lakini….” 

“Mmmh! Usisiseme lakini.” Mzee mmoja ambaye ndiye alikuwa mwenyekiti wa kikao kile alimkatisha mama Annabelle. Kisha akaendelea, “Sasa tumeona picha halisi hapa tuhuma zote zinaelekezwa kwa kijana wetu Martin……” Mzee yule alisita kidogo kisha akapata fundo moja la maji baridi kisha akaendelea, “Kwakuwa Martin mwenyewe yuko hapa hebu tumpe nafasi ya kumsikiliza….” Aliongeza mzee yule na kila nmoja akatikisa kichwa juu chini ikiashiria kuwa wanaunga mkono hoja yake.

Mzee yule yule ambaye anatokea kijiji kimoja na alichotoka Martin na ni mtu anayeheshimika sana kijijini kwao. Alimgeukia Martin, “Martin kijana wangu, tuhuma zote zimekufuata wewe, sasa nataka utueleze nini kilitokea siku ile….” Alimaliza kumuekeza Martin kisha akasubiri majibu.

Martin alivuta pumzi ndefu kisha akawatazama kila mmoja katika kikso kile kisha akaanza, “Awali ya yote niwashukuru nyote kwa kufika hapa ili kutatua mzozo huu kati yangu na mke wangu na mama mke wangu.” Martin alitulia tena kisha anaendelea, “Siku hiyo tulianza safari vizuri kutoka hapa nyumbani kuelekea kujijini kwa aajili ya kusalimia lakini pia kwa shughuli mbalimbali za kijamii kama kawaida yangu. Tukiwa njiani tulikutana na kijana mmoja aaliyetusimamisha nasi tukasimama. Kijana yule alitusalimia mimi na mke wangu kusha akajitambulisha kuwa anaitwa Robert. Baada ya hapo alitueleza kuwa amepata matatizo, watu wamempora kila kitu chake ikiwemo fedha zake na nguo alizokuwa nazo.” Martin alitulia tena na kuvuta pumzi ndefu na kuitoa.

 

Kisha akaendekea, “Nilimuonea huruma sana, akatuomba msaada tumfikishe katika kijiji alichokuwa anakwenda kwakuwa nasi tulimueleza juu ya safari yetu. Pamoja na kumuonea huruma, kuna wakati nilisita nikidha pengine anaweza kuwa jambazi. Kabla sijatoa maamuzi yangu, ilinibidi nipate maoni ya mke wangu na mwanangu. Waliafiki tumsaidie na mimi sikuwa na hiyana nilimruhusu apande garini, alishukuru sana.” Martin aliwaeleza.

Martin alitulia kisha akaendelea kusimulia, “Kijana yule alionekana kuelewana sana na binti yetu, kama mzazi ilinipa wasiwasi na niliwaza, pengine anaweza kuwa mtu wanaeelewana sana na mwanangu tangu muda mrefu lakini kadri walivyokuwa wanazungumza nilibaini kuwa hawakuwa wanafahamiana. Pia nilikuwa na mawazo anaweza kuwa jambazi, kajini wazo hili nalo halikuwa na nafasi sana mwisho niliamini kuwa kijana huyo alikuwa mtu mwema na hakuwa madhara yoyote kwetu.” Martin alitulia, machozi yalianza kumlenga lenga.

Mzee yule ambaye ndiye kiongozi wa kikao kile alimwambia ajikaze kisha aendelee kuwasimulia. Martin alijikaza na kuendelea kuwasimulia. “Tuliendelea na safari yetu ambayo kwa kiasi kikubwa ilitawaliwa na mazungumzo kati ya binti yangu na kijana huyo, maongezi yao yakijikita katika elimu na kumcha MUNGU.” Martin aliweka nukta na kufuta machozi ambayo sasa alishibdwa kuyazuia. 

Martin akiendelea kuwaeleza, “Baadae tulioba gari likitufuatilia jwa nyuma, gali hilo nililitilia shaka baada ya kusimama na kuziba barabara, tuliendelea mbele kifogo likatokea gari jingine na kuziba njia kisha wakashuka wati wanne wakiwa na silaha, walituamuru kushuka garini kisha wakasema wanahitaji kuondoka na mtu mmoja na nilazima awe kijana! Sikutaka kabisa mtu yeyote adhirike, niliwaomba waiache familia yangu kisha wanichukue mimi badala yao lakini wakikataa katakata na kusema kuwa wanahitaji kijana kwa ajili ya kutoa kafala.” Martin alifuta tena machozi na kisha kuendelea, “Waliendelea kusisitiza na wasema kama nitakuwa msumbufu wataiua familia yangu, walinipa chaguo kuchagua kati ya yule kijana na binti yangu mpendwa, Ritha! Hakika ulikuwa wakati mgumu sana katika maisha yangu niliamua kuwaruhusu wamchukue binti yangu Ritha….” Martin alieleza kwa uchungu huku akiangua kilio kama mtoto ndogo.

“Mnaona? Niliwaambia huyu ni mshirikina mkanikatalia. Alimtoa bibti yake mwenyewe kwa ajili ya kafala hapo anajaribu kutupumbaza tu alipanga kila kitu, sasa sitakubali mwanangu pia awe kafara nitaondoka na binti yangu.” Mama yake Annabelle alidakia na kupigilia nsumari wa moto katika moyo wa Martin. 

Wazee wake Martin walijikuta wakimuamini mama yake Annabelle na kushindwa kumuamini kabisa Martin. Kitendo hiki kilimuuma sana Martin akijaribu kuwaelewesha kadri alivyoweza lakini ilishindikana. Annabelle alibeba vilago vyake na kuondoka na mama yake japo kuwa alijitahidi sana kumbembeleza Mkewe (Annabelle) abaki lakini Annabelle hakuekewa kitu alishikilia uamuzi wake wa kuondoka na kuapa kutomsamehe kamwe.

Martin alibaki chini akiwa haamini kinachotokea, akiwa bado katika mshangao alisikia sauti, “Bosi…” Ilikuwa sauti ya mlinzi wake. Alimtazama, alishangaa kumuona akiwa amebeba begi lake, “Samahani bosi wangu, inabidi niondoke pia” Mlinzi huyo alimueleza Martin.

Martin hakujibu kitu alizidi kushangaa tu huku akimsindika kwa macho ya mshangao akitokomea katika upeo wa macho yake. Alisimama na kurejea ndani. Alifika sebleni kwake na kuitazama, aliiona imekuwa kubwa sana unaweza kugawa hata vyumba vitu na kubaki sehemu kubwa ya sebule. Machozi yalikuwa yakitoka mfululizo na hayakuwa na kizuizi chochote, alijitupia kwenye kochi kama gunia la mchele. Kila sehemu aliyoitazama alikuwa akikumbuka tu namna yeye na familia yake walivyokuwa na furaha. Martin alishindwa kuzuia uchungu alionao, alilia sana alimlilia MUNGU wake sana.

Ulikuwa ni mwanzo wa machungu kwa Martin, taarifa zilizagaa kuwa, “Millionaire Martin Okafor ni mshirikina.” Taarifa hizi zilimuumiza lakini hakutaka kupambana nazo kwakuwa alijua fika hata afanye nini kwa uwezo wake hatoweza zaidi sana atajikuta akitenda dhambi ambayo itahalalisha uvumi huo. Alijisemea, “Vita hivi nakuachia eeh Mungu, naomba unishindie.” 

Stanley Ikena kijana ambaye kwa mara ya kwanza katika maidha yake alijikuta akiandamwa na matukio mfululizo. Kwanza ilikuwa siku ile alipokuwa anasafiri kutoka jeshini kwenda kijijini kwso kutumilia jamii kwa mwaka mmoja, akiwa anasubiri usafiri aliporwa kila kitu chake. Haikuishia hapo, lilitokea tukio jingine baya na lililomuachia kumbukumbu ya kufundisha, kushangaza na kusikitisha. Tukio hili lilimkosesha raha sana. Alirudi kwa mjomba wake aitwaye Mr. Jerome ambaye ni mfanyabiashara mkubwa tu jijini Lagos.

Siku moja Stanley aliamua kumueleza mjomba wake juu ya tukio zima lililotokea siku ile alipoaga kuwa anakwenda kutumikia jamii kijijini kwao. Alikwenda Seating room na kumkuta mjomba wake akijisomea gazeti.

“Shikamo mjomba.” Stanley alimsalimia.

“Ooh! Stanley, marahaba uncle kumbe ulikuwepo ndani?” Aliitikia Mr. Jerome.

“Ndiyo sijaenda chuo leo!” Stanley alimueleza mjomba wake.

“Kwanini, unaumwa?” Mjomba wake alimuuliza huku akiacha kusoma gazeti lake.

“Hapana uncle, kuna kitu kinanisumbua tu?” Stanley alijibu kinyonge sana hali iliyomfanya Mjomba wake awe na wasiwasi.

“Au umemaliza pesa?” Mjomba wake aliendelea kumdadisi.

Stanley alitulia kidogo na kuvuta pumzi ndefu kisha kuitoa nje. Alijitengeneza vyema kwenye sofa lenye gharama ya kununua pikipiki aina ya Boxer kadhaa hivi.

“Uncle, pesa ninayo ya kutosha nikimaliza nitakwambia.” Akijibu Stanley.

“Sasa kumbe shida nini? Hebu funguka basi au kam hutaki useme.” Kiasi fulani sauti ya mjomba wake ilionesha kukereka kutokana na kucheleweshwa kupatiwa habari aliyo ihitaji.

“uncle unakumbuka siku nakwenda kutumikia jamii nilikupigia simu nikakwambia kuna tukio lilitokea na nikakwambia nitakueleza nikirudi?” Stanley alianza kufunguka.

Itaendelea........

USIKOSE KUFUATILIA HADITHI HII YA JARIBU LA USHINDI SIKU YA JUMANNE.

Post a Comment

0 Comments