JARIBU LA USHINDI SEHEMU YA 3


ILIPOISHIA............

Annabelle alipoamka alikuta kiasi cha pesa cha shilingi milioni 3 tofauti na ilivyokuwa awali kuwa kila mwisho wa mwezi hupewa milioni 2. Alizichukua zote na kuziweka katika kisanduku chake ambacho hukitumia kuhifadhi pesa zake. Alijiandaa na kisha akachukua ufunguo wa gari lake aina ya Benz na kuondoka kuelekea kwa rafiki yake aitwaye Juliet. 

Walipoonana walikumbatiana kwa kuwa hawakuwa wamekutana kwa muda mrefu sana.

Walianza maongezi yao na Annabelle akamueleza rafiki yake kila kitu juu ya kile kilichotokea hadi mtoto wao akauawa. Juliet alimpa pole rafiki yake na kumshauri kukaa mbali na Martin kwani kuna uwezekano akamuua pia ili ajipatie utajiri, maneno yale yalimuingia Annabelle na akayabeba kama yalivyo.

Anabelle aliporudi nyumbani alianza kutafakari juu ya mambo ambayo aliambiwa na rafiki yake naye alihisi kuwa ni kweli kwa kila kitu alichoambiwa na rafiki yake, hapo hasira na chuki dhidi ya Mumewe iliongezeka.

SASA ENDELEA..........

Njioni mumewe alirejea akiwa na hamu sana na mkewe lakini hakujua ni kwa namna gani mkewe alivyo jazwa sumu. Alifika na kukuta mkewe amelala tofauti na alivyozoea akitazama television. Alienda kuoga na kisha akarejea sebleni, alikaa kwa muda kidogo kisha akanyanyuka na kwenda chumba alicholala mkewe. Alipofika alikuta mkewe amelala kihasara hasara, akahisi damu inamchemka kuliko kawaida, mapigo ya moyo wake yakaanza kumwenda mbio mbio, jogoo la mjini likawika shamba. Martin akamsogelea mkewe pale kitandani na kuanza kumpapasa mkewe mapajani taratibu mkono wake ukielekea kibo na mawenzi, akiwa anakaribia kibo mara mkewe akastuka alipomuona mumewe alimsukuma kwangu. Martin akadondoka chini! 

“Honey nini hiki sasa?” Martin alimuuliza mkewe kwa mshangao.

“Nini kuhusu nini?” Annabelle naye akajibu kwa swali huku akiwa amefura kwa hasira.

“Baby kwanini unaninyima haki yangu?”

“Haki ipi? Nakuuliza wewe muuaji haki ipi?”

“Annabelle wewe ni mke wangu tena wa ndoa na hii ni haki yangu unaninyima kwa miezi mitano sasa why are you doing this to me?” Martin alimlalamikia mke wake. 

“Mke! Haki! Hivi unadhani kwa kwa kile ulichokifanya kwa mtoto wetu bado unayo haki juu yangu? Hapana Martin, huna haki hiyo tena na kwa taarifa yako, huu ni mwanzo tu, utateseka sana.” Annabelle alimueleza mumewe maneno ambayo kwa hakika yalimuumiza sana Martin. Baada ya kumueleza maneno yale Annabelle akachukua mto mmoja kwenda kulala chumba cha wageni. Hili hakulitegemea japo anaelewa wazi kuwa mkewe huyo anamchukia sana lakini hadi kulala vyumba tofauti, hii ilimuwashia taa ya kijani, hakutaka kumzuia alimuacha kisha akarejea kitandani. Alitazama kaptula yake tayari ilikuwa inaunyevu unyevu sehemu ya mbele, akatikisa kichwa kisha akachukua taulo yake na kuingia bafuni kuoga, alipomaliza alijiweka sawa kisha akalala.

Asubuhi ikafika Martin alijiandaa kwa ajili ya kuelekea kazini, alipofika mlangoni alikumbuka kuwa yeye na mkewe hawakulala chumba kimoja, hivyo akaamua kwenda kumjulia hali mkewe, aligonga mlango lakini hakujibiwa aliamua kuufungua. Akiingia ndani ya chumba kile na kukuta mkewe yuko kwenye usingizi mzito huku akijigeuza kuelekea upande mwingine, Martin alitabasamu kisha akaufunga mlango na kuelekea kazini. 

Annabelle alipoamka alijiandalia kifungua kinywa kisha akakumbuka kumpigia mama yake simu. Mama yake alipokea na kumuuliza anaendeleaje.

“Mama naendelea vizuri ila namkumbuka tu mwanangu mama….” Annabelle alianza kulia wakati akimuelezea juu ya hali yake na namna alivyomkumbuka Ruth.

“Mwanangu, Juliet ameniambia kila kitu ni kwanini hukuniambia mapema…. Huyo mwanaume inaonekana wazi ni mshirikina, hizo mali ni kwasababu ya kutoa watu kafara sasa ameamua hadi kumtoa kafara mtoto wake mwenyewe, unbelievable!”

“Mama ninaumia sana kwa kweli, mtoto mwenyewe alikuwa mmoja kama dawa halafu kirahisi rahisi tu anakufa jamanii mamaaa.” Annabelle aliendelea kumueleza mama yake kwa uchungu.

“Pole mwanangu, usijali I've to do something before it's too late….Usijali mwanangu ila naomba uwe makini sana na huyo mwanaume.”

“Sawa mama nitakuwa makini sana.”

Annabelle alimaliza kuongea na mama yake na kisha wakakata simu.

Mama yake Annabelle aliamua kumpigia simu Martin na kuanza kumtukana na kumtuhumu kuwa amemuua mjukuu wake, Martin akijitetea sana lakini hakuna kitu kilichobadilika, mama mkwe huyo aliendelea kumtuhumu kuwa mali zote alizonazo ni kwa sababu alitoa kafara ya watu ili awe tajiri. Hii ilimuumiza sana Martin aliamua kukata simu. Alitaka kupata msaada kutoka kwa mtu, na mtu pekee aliyemfikiria alikuwa ni Juliet!

 

Alichukua funguo za gari na kutoka katika ofisi yake huku akimuelekeza secretary wake kukata mikutano yote aliyokuwa nayo siku hiyo na kuipangia tarehe nyingine.  Aliingia ndani ya gari yake na kuelekea anakofanyia kazi Juliet katika kampuni ya simu ya MTN. 

Juliet alikuwa nje ya jengo la makao makuu ya kampuni ya simu ya MTN, alikuwa akizungumza na mtu mara akaja kijana mmoja ambaye alimueleza kuwa kuna mtu amemuagiza amuite.

“Ni nani?” Juliet alihoji kwa mshangao.

“Simfahamu…Yuko pale kwenye maegesho ya gari.”

“Okey asante…. Naomba uniwie radhi, ngoja nikamuone huyo mtu.” Juliet alikubali wito kisha akamuaga mtu akiyekuwa anazungumza naye na kwenda kumuona mtu aliyeelekezwa kuwa yuko kwenye maegesho ya magari.

Juliet alipofika hakuamini, alikuwa ni Martin, mume wa Annabelle. Hasira zikamjaa, “Unafanya nini hapa?” Juliet alimuuliza Martin kwa hasira.

“Juliet salamu kwanza basi…”

“Hakuna haja ya salamu…. Sikia sema shida yako na uondoke!”

Martin alibaki akidua maana Juliet akiyeko mbele yake muda huo si Juliet yule aliyekuwa akimchangamkia na kumsifia kila wakipokutana. “Anyway, Juliet niko hapa kukuomba msaada!”

“Wa kumuua Annabelle?” Juliet alimuuliza Martin swali gumu na la ajabu sana.

“WHAT?” Martin aliuliza kwa shangao hakuamini alichokisikia kutoka kwa Juliet.

“Ooh! Ulidhani siri yako haitafichuka eeh? Ulidhani hatutajua kuwa wewe ndiye uliyemtoa kafara mwanao mwenyewe ili upate utajiri ulionao sasa na sasa unataka umuue na 7 yangu,hapo umekwama Martin.” Juliet aliongea maneno makavu makavu ambayo yalimduwaza Martin.

“Excuse Me! Juliet, what the hell are you talking about?” Martin aliuliza kwa mshangao.

“Martin, sina muda wa kupoteza na Wewe, kusanya makongoro yako na uondoke hapa sasa hivi…”

“Juli…”

“Martin ondoka haraka au nitaita walinzi, muuaji mkubwa wewe.”

Martin hakuwa na la kufanya aliamua kuingia ndani ya gari yake na kuondoka huku akiwa na machungu moyoni na kichwani mwake maneno kama kafara, muuaji yalizidi kujirudia kichwani mwake. Martin alijikuta machozi yakimtoka, akaanza kulia kwa uchungu huku akimuuliza Mungu kama kweli yeye ni mbaya kiasi hicho. Akiwa kwenye dimbwi la mawazo mala bodaboda akakatiza mbele ya gari yake haraka akaanza kumkwepa na bahati mbaya akaenda kuigonga nguzo ya umeme iliyokuwa upande wa kulia, akazimia hapo hapo.

Martin alipoamka alijikuta yuko juu ya kitanda cha hospitali, alipotazama pembeni yake kulikuwa na chupa ya drip, alipojitazama akaona amefungwa budge maeneo mbali mbali ikiwemo kichwani. Alipotazama mlangoni alimuona nesi akiingia.

“Taratibu utajiumiza, tulia tu acha kuhangaika” Ilikuwa ni sauti ya upole ya nesi.

“Nimefikaje hapa nini kimetokea?” Martin aliuliza kwa shida kwa kuwa alikuwa anahisi maumivu sehemu mbalimbali za mwili wake.

“Umeletwa hapa na waaamaria wema, ulipata ajali ya gari!”

“Ooh! My God nimekumbuka…Daktari yuko wapi?” Martin alimuuliza yule nesi.

“Usijali daktari atafika muda si mrefu.” Nesi alijibu kwa sauti ya kiungwana sana iliyomvutia Martin hata kutamani aendelee kukaa hapo hospitali.

“Je, kuna mtu yeyote ungetaka kuwasiliana naye kumueleza juu ya hali yako?” Nesi alimuukiza Martin.

“Yeah yupo, simu yangu….”

“Hakuna simu iliyoletwa hapa pengine….”

“Wameshaiba wasamaria wema” Martin alijibu kimasihara hadi nesi akajikuta amecheka kama ni mazuri.

“Unavituko sana wewe, usijali nipatie namba za mkeo nimpigie”

Martin akamtajia nesi yule namba za mkewe na kisha akampigia simu na kumueleza kuwa afike hospitali ya Mt. Joseph ili kumuona mumewe.

“Asante sana nesi, unaitwa nani?” Martin alimshukuru nesi yule na kumuuliza jina lake.

“Usijali ni sadaka tu hii, naitwa Sonia” Nesi alijibu kuhu akikagua kagua chupa ya drip.

Baada ya muda daktari alifika na kusalimiana na Martin. “Unajisikiaje?” Daktari aliuliza.

“Najisikia maumivu kiasi katika kichwa, mkono na mgongo” Martin alimuelezea daktari anavyojihisi.

“Ni sawa, hata hivyo hakuna majeraha makubwa uliyopata, nimekufanyia vipimo vyote uko salama hakuna mfupa uliovunjia, uko salama na haya msumivu ni yakawaida kabisa.” Daktari alimuelezea Martin ambaye alijisikia faraja sana kusikia kuwa hakupata madhara makubwa kutokana na ajali aliyopata.

Akiwa bado anazungumza na dakari, Annabelle aliingia akiwa hana hata chembe ya shauku kutaka kujua mmewe anaendeleaje.

“Ooh! Mke wangu, umefika?”

“Hapana naondoka…Kwahiyo hujafa?” Annabelle aliuliza swali lililowashangaza Martin, nesi na Daktari. 


 Itaendelea........

Usikose kufuatilia simulizi hii ya JARIBU LA USHINDI SIKU YA KESHO.

Post a Comment

0 Comments