JARIBU LA USHINDI SEHEMU YA 2


 ILIPO ISHIA.........................

“Baba leo utanipeleka cinema?” Ritha alimuuliza baba yake ikiwa ni ahadi aliyopewa na baba yake kabla hajafanya mtihani wa taifa.

“Oooh! Yeah lazima twende na umwambie mama yako leo ajiandae leo usiku tutakwenda Cinema kuna filamu mpya ya Ken Eric na Yul Edochie waigizaji mnaowapenda”

“Asante baba, nakupenda”

“Nakupenda pia mwanangu” Martin naye alijibu na kumuacha binti yake aende kwa mama yake.

Martin alimuwekea utaratibu binti yake kuwa endapo anataka vitu vya kujifurahisha ni lazima avifanyie kazi, hawezi kuvipata bure tu. Hivyo ndivyo ilivyotekea kabla hajafanya mtihani, Ritha alimuomba baba yake ampeleke kwenye Cinema lakini baba yake alimwambia kuwa utaratibu ni ule ule, nilazima afaulu mtihani kwake ndipo anpekeke Cinema. Utaratibu huu ulimsaidia sana Ritha kufanya vizuri shuleni kwani alijua kwakufanya hivyo basi angepata chochote anachotaka bila maswali.

Alipofika kidato cha tatu alipata likizo ya katikati ya mwaka yaani nusu muhula ambapo awali aliahidiwa akifaulu basi atapelekwa kijijini kupumzika na babu na bibi yake jambo ambalo Ritha alikuwa analisubiria sana.

Siku ya safari iliwadia, na siku hiyo ilikuwa ni mwisho wa wiki yaani jumamosi, walidamka asubuhi na mapema kila mmoja akajiandaa kwa ajili ya safari. Waliingia ndani ya gari yao na kuanza safari kuelekea kijijini kwao.

SASA ENDELEA.............

Ninabell alianza kumchukia sana mume wake kwasababu ya kifo cha binti yao, Ruth. Martin alijitahidi kuomba msamaha kadri alivyoweza lakini ilishindikana, aliamua kumpa muda mkewe akiamini pengine ni kwasababu anapitia wati mgumu sana tika maisha yake baada ya kumpoteza binti yao kipenzi. Martin aliamua kuwa imara kwa ajili ya mkewe na hata yeye pia japo ndani ya moyo wake alikuwa na maumivu makali sana kwa kifo cha binti yao mpendwa. Juna wakati alikuwa akikaa ofisini huinamia meza yake na kuanza kulia kwa uchungu aliokuwa nao lakini akiwa na mkewe au watu wengine, huwa anajionesha kama mtu imara na asiye na asiye na maumivu au majuto yoyote na hii ndiyo ilikuwa sababu ya mkewe kuzidisha chuki dhidi yake.

Baada ya miezi mitatu kupita Martin aliamua kufanya kazi kwa bidii na alimuomba Mungu sana amsamehe na amtie nguvu katika kufanya kazi zake pengine mafanikio yangeweza kumfanya mkewe angalau apoteze mawazo na aanze kujivunia kuwa na mwanaume imara.

Siku moja asubuhi na mapema ikiwa ni mwanzo wa wiki, Martin alidamka kama kawaida yake alijiandaa kwa ajili ya kuelekea kazini. Alifika mezani na kukuta meza nyeupe, alimuita mkewe aliyekuwa anatazama picha ya binti yao, “Mke wangu…Mke wangu…. Annabelle si ninakuita!” 

Mkewe alintazama na kisha akaendelea kutazama picha, Martin alianza kupandwa na hasira kidogo kutokana na dharau aliyooneshewa na mkewe. “Annabelle kwanini hujaniandalia chai wakati unajua kabisa kuwa huwa nakunywa chai nyumbani kabla sijaenda kazini?” Martin alimuuliza mkewe kwa sauti ya ukali kidogo.

“Eeeeh! Ishia hapo hapo muuaji mkubwa wewe….Kimya, kwani jiko hulioni lilipo?” Annabelle alimjibu mumewe ambaye alibaki akidua kwa maneno ya mkewe.

“Annabelle! Ni wewe mke wangu unayasema haya?” Martin hakuamini kabisa alichokisikia lakini huo ndiyo ukweli kuwa mkewe alikuwa amebadilika sana, ilimuumiza sana hali hiyo lakini aliendelea kujitahidi kumuelewa mkewe kuwa bado anawati mgumu. Aliamua kubeba begi lake la kazini na kuondoka.

Martin alifika kazini baada ya dakika 20 na hakika na kuketi katika kiti chake. Alianza kutafakari mambo yaliyotokea nyumbani kwake mapema asubuhi, aliumia sana, alisikia sauti ndani mwake inamwambia, ‘You are not a Victim but a victor.’ Alistuka na kuketi vizuri kwenye kiti chake cha kiboss ofisini kwake, kisha akatabasamu. Akiwa bado katika tabasamu akasikia simu yake ya mezani inaita, akaipokea haraka, “Hallo, Mr. Martin hapa….”

“Ooh! Habari, unaongea na Dkt. Egube Ike, nimekupigia kukutaarufu kuwa niko tayari kufanya kazi na wewe na kwa kuanza nitakupatia mradi wa 2.5 Billion nahitaji mradi ukamilike kwa haraka sana.”

“Sir, are you serious?” Martin aliuliza kqa mshangao kwakuwa hakutarajia alichokisikia kwenye simu hiyo. Alifurahi na kumshukuru sana Dkt. Egube. Alimuita secretary wake na kumpa maelekezo na mara moja kazi ikaanza. 

Jioni alirudi nyumbani akiwa hoi na njaa pia, alimkuta mkewe anatazama television, alimsalimu mkewe lakini aliambulia msonyo wa karne akajiongeza mwenyewe kimya kimya hadi mezani ambako nako hakukuta chakula chochote licha ya kuacha pesa za kutosha. Alidhani pengine chakula kipo jikoni, alipofika alikuta kulikuwa na dalili kuwa kulipikwa lakini hakuna kilichobaki kwa ajili yake! Alitaka kwenda kumuuliza mkewe lakini akaona haitakuwa sawa kufanya hivyo na itasababisha ugomvi kitu ambacho hakutaka kitokee.

Alirudi sebleni ambako alichukua kibegi chake na kuingia ndani, akijitupa kitandani taratibu usingizi ukaanza kumnyemelea, hajutaka hilo litokee mapema hivyo, alioga na kisha kubadili nguo. Akachukua funguo za gari lake na kuelekea nje alikolipaki, aliingia na kisha kuondoka taratibu, akakamata barabara iliyokuwa inaelekea mjini huku akisikiliza mziki wa injili toka kwa msanii maarufu nchini Nigeria. Alifika kwenye mataa na kusimama baada ya taa nyekundu kuwaka, baada ya dakika kama moja taa ya kijani iliwaka naye akaweka gia ya kuondokea na kupinda kushoto hadi katika mgahawa maarufu F&J restaurant, mgahawa unaomilikiwa na ndugu wawili, aliagiza chalula apendacho na kisha baada ya dakika kadhaa akiwa anaendelea kula aliagiza chakula kingine kwa ajili ya mkewe, japo jikoni kulikuwa kuna dalili kuwa kulipikwa, aliamini pengine mkewe alimpikia mlinzi.

Alibeba kile chakula na kurejea nyumbani kwake, akimkuta mkewe bado anatazama television, hakutaka kuongea nae maneno mengi sana, akimuekea kile chakula mezani na kumwambia, “Mke wangu chakula chako kiko hapa mezani, usiku mwema.” 

Mkewe wala hakujibu kitu na Martin alilizoea hilo kutoka kwa mkewe hivyo hakujisumbua sana.

Aliingia kulala na baada ya muda mkewe aliingia chumbani. Martin alikumbuka kuwa kuna habari njema hajamueleza mkewe hivyo ikabidi amueleze, “Mke wangu nimekumbuka kitu, leo nimepata contract ya 2.5 Billions…Mungu amekuwa mwema sana kwetu.” Martin alimueleza mkewe lakini badala yake alipokea msonyo ule ule wa karne kisha mkewe akavuta shuka lake na kugeukia ukutani. 

Asubuhi Martin mtu wa kazi aliamka na kama kawaida yake alijiandaa na kupita mezani lakini hakukuta chochote akaendelea na safari yake kuelekea kazini hakutaka kumuamsha mkewe alimuachia fedha kwa ajili ya chakula na matumizi yake binafsi ikiwa ni kawaida yake kumpa mkewe kila mwezi kiasi cha million 2 kwa ajili ya matumizi yake binafsi kwa kuwa hafanyi kazi na alikataa kufanya kazi mara baada ya kumpoteza mtoto wao kwa madai kuwa anahitaji muda ili awe sawa.

Annabelle alipoamka alikuta kiasi cha pesa cha shilingi milioni 3 tofauti na ilivyokuwa awali kuwa kila mwisho wa mwezi hupewa milioni 2. Alizichukua zote na kuziweka katika kisanduku chake ambacho hukitumia kuhifadhi pesa zake. Alijiandaa na kisha akachukua ufunguo wa gari lake aina ya Benz na kuondoka kuelekea kwa rafiki yake aitwaye Juliet. 

Walipoonana walikumbatiana kwa kuwa hawakuwa wamekutana kwa muda mrefu sana.

Walianza maongezi yao na Annabelle akamueleza rafiki yake kila kitu juu ya kile kilichotokea hadi mtoto wao akauawa. Juliet alimpa pole rafiki yake na kumshauri kukaa mbali na Martin kwani kuna uwezekano akamuua pia ili ajipatie utajiri, maneno yale yalimuingia Annabelle na akayabeba kama yalivyo.

Anabelle aliporudi nyumbani alianza kutafakari juu ya mambo ambayo aliambiwa na rafiki yake naye alihisi kuwa ni kweli kwa kila kitu alichoambiwa na rafiki yake, hapo hasira na chuki dhidi ya Mumewe iliongezeka.


ITAENDELEA...........

_________________

Post a Comment

0 Comments