![]() |
HASEENA PARKER |
Pengine uliwahi kusikia ama uliwahi kuona filamu kuhusu
mwamba huyu kutoka India aitwaye Haseena Parker, kama hukuwahi kusikia au
kuona, usiwe na shaka leo unatoma simulizi kumuhusu mwanamama huyu amabaye
alitikisa mji wa Mumbai. Haseena Parker aliingia moja kwa moja katika biashara
haramu na magenge ya kihalifu baada ya mumewe Ibrahim Parkar kupigwa risasi
mnamo Mwaka 1991 na jamaa aliyeitwa Arun Gawli akishirikiana na genge lake. Baadae
yalitokea mauaji katika hospitali ya JJ, Shambulio hili la mauaji lilipangwa na
kutekelezwa na Dawood Ibrahim kaka wa Haseena kulipiza kisasi baada ya kifo cha
shemeji yake.
![]() |
Haseena Parker akiwa kwenye sherehe |
Baada ya kifo cha mumewe, Haseena alihamia kwenye kasiri
lake jipya, liitwalo Gordon Hall Apartments huko Nagpada na huko ndiko alikuwa
akiendesha shughuli zake za kihalifu. Aliipenda nyumba sana nyumba hiyo na
ndipo alipoivunja na kuijenga upya na hakuna hata mmoja aliyethubutu
kulalamika.
Haseena alikuwa na ushawishi mkubwa sana nchini India kiasi
kwamba akawa anahusika katika masuala mbalimbali na kuwa kama daraja la
makampuni ya ujenzi ambayo aliyasaidia kupata vibali mbalimbali vya ujenzi wa
makazi hasa katika maeneo ambayo yalikaliwa na watu maskini chini ya miradi ya
SRA. Parkar pia alihusika katika kujadili kuhusu haki miliki za filamu za
Bollywood, haswa filamu zilizokuwa zinakwenda kuuzwa Urusi ya Kati na nchi za
Ghuba.
![]() |
Dawood Ibrahim kaka wa Haseena Parker |
Haseena Parkar alizaliwa katika wilaya ya Ratnagiri, Maharashtra
katika familia ya Kiislamu ya Marathi. Baba yake Ibrahim Kaskar alikuwa mkuu wa
polisi katika Idara ya Polisi ya Mumbai na mama yake Amina Bi, alikuwa mama wa
nyumbani. Haseena Parkar alikuwa mdogo wake Dawood Ibrahim. Katika jumla ya watoto
12 wa Bwana Ibrahim, Haseena alikuwa mtoto wa saba na Dawood Ibrahim alikuwa
mtoto wa tatu.
Mara tu baada ya Dawood ambaye alikuwa ni kaka yake na mkuu
wa magenge ya kihalifu kukimbilia Dubai, Haseena alifuata nyayo za kaka yake
huyo na kuingia katika ulimwengu wa uhalifu. Aliwaeleza polisi na mahakama kwamba hakuwa akiwasiliana
na kaka yake Dawood Ibrahim lakini baadae yeye ndiye alichukua biashara za kaka
yake katika jiji la Mumbai na kuzisimamia kwa niaba yake. Vyanzo mbalimbali
vinadai kuwa mwanamama huyu alikuwa na utajiri wa 5000 Crores. kila Crore 1 inawakilisha milioni 10 piga
hesabu hapo ujue ni mali kiasi gani alizokuwa anamiliki mwanamama huyu na hizo
ni mali ambazo serikali haikuwa inafahamu.
Haseena alipoteza mwanawe mkubwa aliyeitwa Danish katika
ajali ya barabarani mnamo 2006 kwenye barabara kuu ya Mumbai-Goa alipokuwa
akirejea kutoka mjini Goa. Danish alikuwa akipendwa sana na mjomba wake, Dawood.
Kutokana na shughuli zake, Haseena ndiye mwanafamilia ya Dawood
Ibrahim aliyefuatiliwa sana na polisi kupita mwanafamilia yeyote, na kila mara
alikuwa kwenye macho ya polisi wakimfuatilia hatua kwa hatua. Alikuwa na kesi zaidi
ya 88 kwa mkupuo ndani ya mahakama ambazo zote zilimhusisha yeye .
Pasipoti ya Haseena yenye No A2745364 iliyotolewa Aprili 5,
1997, ilikuwa halali hadi Aprili 6, 2007. Hata hivyo, Februari 14, 2005, baada
ya kutembelea Mumbai Crime Branch ( MCB) baada ya kualikwa kwa mahojiano, pasi
hiyo ya kusafiria ilifutwa. Alipotuma ombi la kupata pasi mpya, alinyimwa
pasipoti hiyo kutokana na shughuli zake za uhalifu na uhusiano mkubwa aliokuwa
nao na kaka yake, Dawood Ibrahim.
Mnamo Julai 6, 2014, Haseena Parker alifariki baada ya
kupatwa na mshtuko wa moyo, akiwa na umri wa miaka 55. Taarifa zinadai wakati
umauti unamkuta alikuwa akifunga kwa ajili ya Ramzan. Haseena aliacha watoto
watatu, binti wawili na wakiume mmoja.
![]() |
Cover ya filamu ya HASEENA |
- Shraddha Kapoor as Haseena Parkar
- Siddhanth Kapoor as Dawood Ibrahim
- Priyanka Setia as Public Prosecutor Roshni Satam
- Ankur Bhatia as Ibrahim Parkar, Haseena's husband
- Feroz Ali Khan as Ghulam Memon
- Samar Jai Singh as Inspector Ranbir Likha
- Rajesh Tailang[9] as Advocate Shyam Keswani
- Daya Shankar Pandey as Police Inspector
0 Comments